• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WANANCHI CHIGELA WAMSHUKURU MHE. SAMIA

Posted on: August 10th, 2023

Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO

Septemba 10.2023

 

Wananchi wa Kata ya Chigela Wilayani Gairo, wamempongeza na kumshukuru Mhe. Dakta Samia Suluhu Hassan, Rais wa awamu ya Sita wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwapatia kiasi cha Shilingi 528,945,425.00 (Milioni miatano ishirini na nane, laki tisa arobaini na tano mianne ishirini na tano) za ujenzi wa miundombinu shule mpya ya Sekondari ya Kata hiyo.

Wametoa shukrani zao hivi karibuni waliposhiriki kwenye zoezi la kusafisha eneo na kuchimba Msingi kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya shule hiyo ili kuwezesha wataalam kwa Idara ya Miundombinu na Mandeleo vijijini kuweka michoro tayari shughuli za ujenzi kuanza mara moja.

Akimwakilisha Diwani wa Kata ya Chigela ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Rahel Nyangasi, Diwani wa Kata ya Magoweko Mhe. Ibrahim Selubunga Mmbwana alisme, Mhe. Dakta Samia , amefanya jambo kubwa sana la kihistoria kwa Wakazi wa Kata hiyo na kuongeza kuwa; kukamilika kwa ujenzi wa Shule hiyo ya Sekondari ya Kata ni ukombozi kwa wanafunzi wa Vijiji vinavyounda Kata hiyo ya Chigela.  

“Kwa niaba ya Diwani wa Kati hii ya Chigela, ambaye ndiye Mwenyekiti wetu wa Halmashaur ya Wilaya ya Gairo, nachua fursa hii kuungana na Wananchi wenzangu kumpongeza na kumshuru Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuondoa changamoto za Sekta ya Elimu katika Wilaya yetu ya Gairo”. Alisema.

(Jengo la vyumba 3 vya madarasa lililojengwa kwa nguvu za Wananchi)

Akasema “Halmashauri ilipokea jumla ya Shilingi Milioni miatano ishirini na nane ambazo zimeelekezwa kutekeleza mradi wa ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Kata ya Chigela, Shule hii itakuwa ya kisasa kabisa kutokana na muonekano wake utakavyokuwa baada ya ujnezi kukamili kwani imebeba miundombinu yote muhimu. Na hii itapunguza adha kwa watoto wetu kutembea umbali mrefu kwenda kata za jirani kupata elimu ya Sekodari”. Alifafanua.

(Jengo la vyumba 3 vya madarasa lililojengwa kwa nguvu za Wananchi)

Naye mwenyekiti wa CCM kata ya Chigela Ndg. Ibrahimu Munga alisema Serikali ya Chama Cha Mapinduzi inatambua adha mbalimbali zinazowapata Wananchi wa Kata hiyo; hivyo juhudi zinafanyika kuhakikisha Wananchi wanaondokana na kero zinazokuwa kikwazo katika kuleta maendeleo hususani Sekta ya Elimu Awali, Msingi na Sekondari.

Kwa upande wake Mweyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Ngiloli Ndg.Dani Samsoni; alisema kuwa Wananchi wa Kata hiyo walipokea kwa heshima kubwa taarifa za mgawo huo wa fedha na kwamba wameamua kujitokeza kujitolea kufanya kazi mbalimbali za awali za kuandaa eneo na kuchimba msingi ili kazi za ujenzi zianze haraka.

“Ninamshukuru sana Mhe Rais kwa kutuona na kusikia kilio chetu Wananchi wa Chigela, hatimaye ametuletea fedhza kiasi cha Sh. milioni 528.945, za ujenzi wa Sekondari Mpya ya Kata. Nasisi tumeamua kutoa shukrani zetu kwa vitendo kuja kujitolea nguvu kazi, ya kusafisha eneo na kuchimba msingi kwa ajili ya shughuli za ujenzi kuanza mara moja”. Alifafanua Ndg. Mwenyekiti huyo wa Serikali ya Kijiji cha Ngiloli.

Kwa kipindi kirefu Kata hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Diwani Nyangasi imekuwa ikikabiliwa na tatizo la ukosefu wa Shule ya sekondari hali ambayo iliwalazimu Wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata shule katika kata ya Kibedya na Magoweko.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Wilaya ya Gairo Bi. Petronila Wakurila, fedha hizo zitatekeleza ujenzi wa Vyumba 8 vya Madarasa, Jengo la Utawala, Maabara 3 za Kemia, Fizikia na Baiyolojia, Maktaba, Jeno la Tehama, Matundu 8 ya vyoo, kuweka mfumo wa maji na kichomea taka.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa