• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WASHAURIWA KUACHA KUKAA VIJIWENI, KUBUNI MIRADI YA KIUCHUMI.

Posted on: June 25th, 2021

Na. Cosmas M. Njingo (AFISA MAWASILIANO GAIRO DC)

Vijana Wilayani Gairo wameshauriwa kuwa wabunifu katika kuibua miradi mbalimbali ya kiuchumi waweze kuzalisha mali sambamba na kutumia fursa za mikopo kwa vijana zinazotolewa na Halmashauri badala ya kukaa vijiweni kucheza bao, kunywa pombe na kujiingiza katika vitendo vya kihalifu ambavyo vinaweza kuathiri afya zao.

Ametoa rai hiyo Mkuu wa Wiaya ya Gairo Mhe. Jabir Omary Makame hivi karibuni alipokutana na kikundi cha Rubeho Transporters cha Vijana waendesha boda boda waliopewa mkopo wa pikipiki 10 na Halmashauri ya Wilaya ya Gairo ili waweze kujiongezea kipato kwa kujiajiri.

“Ushauri wangu kwa vijana wote ni kwamba muache kukaa vijiweni na kupoteza muda pasipo kufanya shughuli za uzalishaji mali, tumieni fursa zilizopo ili mjikwamue kiuchumi kwa kujiunga katika vikundi na kubuni shughuli za kiuchumi ili muweze kuendesha masiha yenu”. Alisema Mhe. JOM.

DC. JOM alisema kuwa Serikali kupitia Halmashauri imekuwa ikitoa fursa za mikopo kwa vikundi mbalimbali vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu ambapo alifafanua kuwa Mamlaka za Serikali za Mitaa zina wajibu wa kutenga asilimia kumi (10) ya mapato yanayo kusanywa kutoka kwenye vyanzo  vya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vilivyo sajiliwa.

“Vijana wenzenu wa Rubeho Transporter waliamua kujiunga katika kikundi wakaomba mkopo Halmashauri kwa kufuata taratibu zote, na baada ya Halmashauri kujiridhisha kuwa kikundi kimesjiliwa na kinakopesheka wakapata asilimia nne (4%) za mapato ya ndani na leo hii wamejikwamuwa”, alibainisha

Rubeho Transporters ni kikundi cha vijana kumi walio ungana kwa pamoja na kupewa mkopo wa Shilingi milioni ishirini na tatu na laki tano (23,500,000) ikiwa ni sehemu ya asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya kuwezesha kikundi hicho kununua pikipiki kumi ambazo zinatumika kibiashara.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bwana Isaya Mihinzo alisema mkopo huo hauna riba na kwamba marejesho yake yatafanyika katika kipindi cha mwaka mmoja hadi kufikia 2022 ili kutoa fursa kwa vijana wengine ambao wanatamani kutumia fursa hiyo kwa ajili ya kujiari na kupata kipato.

“Katika mwaka wa fedha 2020/2021 moja ya vikundi vilivyonufaika na sharia na kanuni hizi ni kikundi cha Vijana cha Rubeho Transporters kilichopo kata ya Rubeho chenye wanachama kumi, kikundi hiki kilianzishwa mwaka 2020, hivyo Halmashauri ilitoa mkopo wa shilingi milioni ishirini na tatu na laki tano kwa mashariti ya kulipa mkopo huo ndani ya kipindi cha mwaka mmoja bila riba yoyote”, alifafanua Bwana Mihinzo.

Ilielezwa kuwa hadi sasa kikundi hicho tayari kimesha rejesha kiasi cha Shilingi milioni sita laki tano na ishirini elfu, sawa na shilingi milioni moja, laki tisa na hamsini na nane elfu mia tatu thelathini na tatu na senti thelathini na tatu kwa mwezi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa