• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WATAALAM WA AFYA, UKIMWI, MARALIA TOKENI MWENDE KWA WANANCHI

Posted on: April 22nd, 2024

Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO

Aprili 21. 2025 Wataalam wa Afya na Lishe Wilayani Gairo, wametakiwa kuongeza juhudi za utoaji wa Elimu kwa Umma kuhusu maswala ya Lishe, matumizi sahihi ya vyandarua ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Malaria, pamoja na kuhamasisha Wananchi kujitokeza kuchangia Damu kwa ajili ya kusaidia wenye uhitaji na upimaji wa Virusi vya UKIMWI ka hiari.

Rai hiyo imetolewa na Ndg. Godfrey Mnzava, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa alipokuwa akitembelea mabanda ya shunguli za Lishe, Malaria, UKIMWI na damu salama wakati wa kukagua na kuweka jiwe la msingi kwenye Zahanati ya Kijiji cha Ng’holonngo Kata yas Madege Tarafa ya Gairo, Aprili 21.2024.

“Hiongereni kwa kazi nzuri mnayoifanya, lakini niwaombe msikae ofisini, tokeni mwende kwa Wananchi mkatoe elimu juu ya umuhimu wa Lishe Bora kwani Mhe. Rais Samia amewekeza Ferdha nyingi katika kuhakikisha afua za lishe zinatekelezwa kikamilifu, hivyo ni bora kuhakikisha mnawafikia Wananchi na kuwapa elimu hiyo”. Alisema Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa.

Akiwa katika banda la kuzuia maambukizi ya Malaria kiongozi huyo alisema Wananchi wanapaswa kufahamu matumizi sahihi ya vyandarua ambavyo vinatolewa na Serikali kwa lengo la kuzuia kuenea kwa ungonjwa huo kwani wapo baadhi ya Wananchi wamekuwa wakitumia vyandarua kwa shughuli tofauti na ilivyokusudiwa  huku akitaja matumizi hayo kuwa ni ufugaji wa kuku, uvuvi na wengine kutumia vyandarua kuzuia kuku kuharibu bustani za mboga mboga.

Kuhusu damu salama Kiongozi huyo amewataka Wataalam hao kuweka mikakati  na kuongeza juhudi za  kuwafikia Wananchi wengi zaidi na kuwapa hamasa ili watambue umuhimu wa kuchangia damu kwa lengo la kupunguza vifo na kuokoa maisha ya  Watoto na Wanawake Wajawazito wakati wa kujifungua..

Mwenge wa Uhuru umepokelewa Wilayani Gairo Aprili 21.2024 ukitokea mkoani Tanga, ambapo utakimbizwa, kuona, kuzindua, kuweka mawe ya msingi na kufungua jumla ya miradi 9 yenye thamani ya shilingi 1,594,217,370.12, huku kauli mbiu ya mwaka huu ikiweka msisitizo katika shughuli za utunzaji wa mazingira na uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika kuanzia mwezi Oktoba hadi Novemba 2024.

“Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu”

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa