• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WATAKIWA KUKUSANYA USHURU WA MIFUGO, NYAMA, KATA YA MKALAMA

Posted on: September 2nd, 2022

Na. Cosmas M. Njingo. Gairo Morogoro

Sept.3.2022


Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Gairo Mhe. Andrea Sendeha amemwagiza Afisa mifugo wa Mamlaka ya Mji huo kuhakikisha anasimamia swala la ukusanyaji wa mapato kupitia ushuru wa mifugo na ukaguzi wa nyama katika kata ya Mkalama.

Sendeha ametoa agizo hilo wakati wa kikao cha Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Mamlaka ya Mji Mdogo cha kujadili taarifa za mwezi Julai 2022, kilichofanyika katika Ukumbi Mdogo wa Mikutano wa Halmashauri Septemba 2.2022.

“Ukipita huko mitaani kwenye Kata ya Mkalama mifugo ipo mingi, nyama zipo za kutosha kila mahali, lakini taarifa ya mapato inayotolewa kwenye vikao vyetu haikisi ukweli uliopo kwenye Kata ya Mkalama.” Alisema Mhe. Sendeha.

Katika kipindi cha mwaka wa Fedha unaoanzia Julai Mosi 2022 hadi Juni 30. 2023 Mamlaka ya Mji Mdogo imekisia kukusanya kiasi cha Shilingi 119,000,000 (Milioni mia moja kumi na Tisa) kutoka kwenye vyanzo mbalimbali katika Kata tano (05) za Mamlaka ya Mji, ambapo hadi kufikia mwezi Julai 30 2022 imekusanya kiasi cha Shilingi Milioni Saba, miatisa na thelathini elfu mia Saba (7,930,700) sawa na asilimia 6.66.

Mchanganuo wa Makisio ya makusanyo hayo kwa kila kata umezingatia upatikanaji wa mapato kupitia vyanzo mbalimbali ambapo kwa mwaka wa Fedha 2022/2023 Kata ya Magoweko inakisia kukusanya jumla ya Sh.40, 000,000 ambapo hadi kufikia Julai 30 2022 kiasi cha Sh.3, 215, 300 kimekusanywa (8.04%).

Kata ya Gairo ilikisiwa kukusanya kiasi cha Shilingi 30,000,000 ambapo kwa mwezi Julai 2022 imakusanya jumla ya Shilingi 3, 239, 400 sawa na asailimia 10.8. Wakati Kata ya Ukwamani ilipanga kukusanya Shilingi 30, 000,000 anbapo imekusanya shilingi 930,000 kwa mwezi Julai 2022 (3.10%)

Aidha Kata ya Mkalama iliweka makisio ya kukusanyo kiasi cha Shilingi 7,000,000 kufikia June 2023 na kwamba katika kipindi cha mwezi Julai 2022 Kata hiyo imefikia asilimia 4.66 ya makusanyo hayo kwa kukusanya jumla ya shilingi 220, 000.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa