• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WATUMISHI IDARA YA UJENZI WAREJESHWA KAZINI, WAWILI WAFUKUZWA KATIKA UTUMISHI WA UMMA .

Posted on: June 10th, 2021

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Gairo limewafukuza kazi Mratibu wa Elimu Kata na Tatibu Afya, kwa tuhuma za utoro kazini, pamoja na kuwarejesha kazini watumishi wengine watano wa idara ya ujenzi waliokuwa wamesimamishwa kwa tuhuma za matumizi makubwa ya ujenzi katika mradi wa mabwalo mawili ya Wasichana shule ya sekondari Gairo, jambo ambalo ilidaiwa kutoendana na uhalisia wa ubora wa majengo hayo tofauti na thamani ya pesa iliyotumika.

Uamuzi huo umetolewa Juni 10, 2021, na Mhe. Rahel Nyangasi, ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri, katika kikao cha Kawaida cha Baraza la Madiwani kujadili taarifa za maendeleo kwa kipindi cha robo ya tatu cha Januari hadi Machi 2021, kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo.

Awali kabla ya kusoma maamuzi katika Baraza hilo lililohudhuriwa na Wataalam mbalimbali wa Halmashauri wakiwepo wananchi, Baraza lilijigeuza kama Kamati ili liweze kupitia na kujadili mashauri ya kinidhamu dhidi ya watumishi hao na baadaye kurejea katika mfumo wa Baraza na kutaja maazimio ya kamati mbele ya Baraza.

 Alisema “Kamati imeridhika kuwa Mwalimu Laurence Mwamondo ambaye alikuwa mratibu wa Elimu kata, pamoja na Ndugu Malowa Malowa kuwa ni watoro kazini kwa muda mrefu, kama vile haitoshi hakuna mawasiliano ya moja kwa moja kuwapata hewani hivyo kuiwia vigumu kamati iliyoundwa kuwachunguza kuwapata, kwa maana hiyo natangaza kuwa Baraza hili limewaondoa rasmi katika utumishi wa Umma”.

Akitaja uamuzi huo Mhe. Nyangasi amesema Baraza hilo limefikia maamuzi ya kuwaondoa kazini watumishi hao wawili kutoka idara ya Elimu na Idara ya Afya kwa tuhuma za utoro kazini baada ya Mamlaka ya nidhamu kujiridhisha pasipo na shaka kuwa watumishi hao wameshindwa kutii taratibu, kanuni na sharia za kazi na kuamua kuto onekana kazini kwa muda mrefu pasipo taarifa yoyote.

Watumishi wanne wa idara ya ujenzi waliorejeshwa kazini ni pamoja na Bwana Nassoro Kindamba (Fundi Sanifu Mkuu Mwandamizi), Bwana Josephat Lyombo (fundi sanifu), Bwana Majija Izengo (Fundi Sanifu) pamoja na Bwana Boniphace Chama (Mkadiriaji Majengo).

“Watumishi hawa wa idara ya ujenzi kimsingi tuhuma dhidi yao hazina mashiko, walisimamishwa kazi kwa muda mrefu lakini hakuna hatua za kiuchunguzi zilizo fanyika huku wakiendela kula mshahara wa serikali, hivyo Baraza limeamua warejeshwe kazini na waendelee na majukumu yao ya kuwatumikia Wananchi” alifafanua Mhe. Nyangasi.

Kwa upande mwingine Baraza hilo pia limewafutia tuhuma watumishi wengine watatu wa Idara ya Elimu Msingi baada ya Kamati ya uchunguzi iliyopewa majukumu ya kuchunguza tuhuma ya kujihusisha na wizi wa mitihani ya Taifa ya darasa la saba mwaka 2020, kutowakuta na hatia dhidi ya tuhuma hiyo.

 “Kwa Mamlaka niliyopewa kwa mujibu wa sheria za Baraza la Madiwani leo tarehe 10 Juni 2021, natangaza kuwafutia tuhuma ya wizi wa mitihani  Afisa Elimu Msingi Wilaya, Ndugu Zakayo Mlenduka, Afisa Elimu taaluma msingi Bi. Digna Matunda na Ndugu Yusuph Mandia, afisa taaluma msingi”, alitangaza.

Maafisa hao kutoka idara ya elimu msingi walikuwa wakikabiliwa na tuhuma ya wizi wa mitihani ya Taifa ya Darasa la saba iliyofanyika mwaka jana 2020, lakini hata hivyo haijathibitika wazi ukweli wa tuhuma hizo hali iliyo sababisha Baraza hilo kuwafutia tuhuma dhidi yao na kuwataka waendelee kuchapa kazi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa