• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAWEKEZAJI GAIRO WAMSHUKURU RAIS SAMIA KA KUWEKA MAZINGIRA WEZESHI YA UWEKEZAJI

Posted on: April 28th, 2024

Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO

Aprili 27.2024

Kwa niaba ya wawekezaji wenzangu wa hapa Gairo, tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu kipenzi Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na kutambua umuhimu wetu katika kuongeza Uchumi wetu binafsi na jamii kwa ujumla.


Shukrani hizo zimetolewa na Bw. Edes Mziwanda Mkazi wa Gairo na Mmiliki wa Nyumba ya kulala wageni ya J5, mbele ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024, Ndg. Godfrey Mnzava wakati wa mbio za mwenge wa Uhuru 2024 zilipofika kukagua na kuona shughuli za maendeleo zinazotekelewa na sekta binafsi.

Akitoa taarifa za utekelezaji wa Mradi huo, Bw. Mziwanda  alimwambia Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kuwa, ujenzi wa Mdadi wa Nyumba ya kulala Wageni ya J5 ulianza kutekelezwa mwaka 2017 baada ya kuonekena kuwepo na mahitaji makubwa ya Nyumba za kulala wageni kutokana na kasi ya ukuaji wa Mji wa Gairom.

“Ndg Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaja 2024, utekelezaji wa mrdai huu ulianza mwaka 2017, hii ni baada ya kuona kuwa kuna mahitaji makubwa ya huduma za malazi kutokana na mwingiliano wa shughuli za kijamii ambazo zimesababisha kasi katika ukuaji wa mji wa gairo”. Alisema Muwekezaji huyo.

Mradi wa ujenzi wa Nyumba ya kulala Wageni ya J5 upo katika kitongoji cha Ukwamani kata ya Ukwamani Tarafa ya Gairo, ambapo jengo la nyumba 11 vyq kulalam huku ukitarajiwa kuwa na tija kubwa kwa Wakazi wa Gairo kutokana na kuzalisha ajira mbalimbali sambamba na kukuza kipato cha mmiliki na Wananchi wengine.

“Ni matarajio yangu kuwa Mradi huu ukikamilika na kuanza kutoa huduma utakuwa na faida kubwa ndani ya Wilaya yetu, ikiwepo kutoa huduma bora za malazi kwa wageni,kuoongeza ajira kwa wananchi hasa vijana na Wanawake, kuongeza mapato ya Serikali kupitia ushuru na kodi mbalimbali pamoja na kukuza uchumi wa Wilaya yetu kutokana na mzunguko mkubwa wa fedha kuendelea kuwepo ndani ya Wilaya ya Gairo” alisema Muwekezaji huyo

Kwa mujibu wa Mziwanda, ujenzi wa Nyumba hiyo ya kulala wageni umegharimu kiasi cha Shilingi 180,000,000.00 hadi kukamilika kwake, kati ya hizo fedha binafsi za mwekezaji ni Shilingi 140,000,000.00 na Shilingi 40,000,000.00 ni za mkopo kutoka Benki

Mbio za mnwenge wa uhuru 2024 zinaongozwa na kauli mbiu inayoisema “Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu”

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa