• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAZIRI OR TAMISEMI APITISHA SHERIA NDOGO YA KUDHIBITI SUMUKUVU.

Posted on: July 2nd, 2024

Na Cosmas Mathias Njingo GAIRO

Julai 2.2024

Miezi michache baada ya Baraza la Wahe. Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya Gairo kuridhia na kupitisha Sheria ndogo ya halmashuri ya kudhibiti Sumukuvu nabaadae kuwasilishwa Ofisi ya Rais Tamisemi kwa ajili ya kupata kibali cha Waziri. Waziri mwenye dhamana hiyo ameridhiana kusaini sheria hiyo ianze kutekelezwa.

Julai 2. 2024 kilifanyika kikao kazi kati ya ujumbe kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi kwa ushirikiano wa Wizara ya Kilimo na Umwagiliaji na kuwakutanisha Maafisa Watendaji wa Kata kwa lengo la kuwajengea uwezo Maafisa hao kutambua matakwa ya sheria na adhabu zake dhidi ya watakaoenda kinyuma na sheria hiyo.

Afisa Kilimo Mkuu kutoka OR Tamisemi, Dkt. Rehema Mdendemi, alisema wakati wa kikao jhicho kuwa Waziri mwenye dhamana alipokea mapendekezo yaliyotolewa na Baraza la Waheshimiwa, baada ya kuipitia kwa kina ameridhia kuisaini ili ianze kutumika kwa lengo la kudhibiti vitendo vinavyosababisha uwwepo wa Sumukuvu kwenye Mazao

“Waziri ameridhia na kusaini sheria hii, nasi tumekuja tupitishane hatua kwa hatua kujua nini kilichomo, ili ikawe rahisi kwetu sote kuitekeleza. Uzuri ni kwamba watunzi wa Sheria hii ni ninyi wenyewe kwani mchakato wa kukusanya maoni ulianzia ngazi za vijiji na Kata kabla ya kufika Halmashauri”. Alisema Dkt. Mdendemi.

Naye Afisa Kilimo Mkuu, Wizara ya Kilimo na Umwagiliaji Bi. Esther Mwasango, aliwaambia Watendaji hao kuwa Sumukuvu ni tatizo kubwa nchini, na nijanga la Kitaifa na kuongeza kuwa endapo Wananchi hawatazingatia kanuni bora za uhifadhi wa mazao madhara yake ni makubwa kwa afya za Binadamu, hivyo sheria hiyo imekuja wakati muafaka ili kuchukua hatua za kukomesha madhara yanayotokana na Sumukuvu kwenye vyakula.


“Halmashuri iliamua kutengeneza Sheria ndogo, ambayo itatumika kudhibiti vitendo vinavyosababisha sumukuvu kwenye mazao na kuleta madhara kwa afya ya binadamu, na hapa wapo Watendaji wa Kata zote, lengo ni kujua dhabu zipi zinapaswa kutekelezwa endapo mwamanchi yoyote atakiuka matakwa yaliyotajwa na Sheria hii”. Alisema Mtaalam huyo.

Mchakato wa uundwaji wa Sheria ndogo hiyo ya Halmashuri ya kudhibiti sumukuvu kwenye mazao ulianzia ngazi za vijiji kwa Wananchi kushiriki kutoa mapendekezo ya rasimu ya sheria hiyo, kujadiliwa kwenye vikao vya maendeleo vya kata na baadaye kuwasilishwa kwenye Baraza la Madiwani kisha kupelekwa kwa Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi ambaye ameridhia mapendekezo ya Sheria hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa