• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

ZIUNDWE SHERIA NDOGO KUWABANA WAZAZI WASIOCHANGIA CHAKULA MASHULENI

Posted on: July 11th, 2022

(wajumbe wa Kamati ya Lishe Wilaya, katika kikao cha Kamati Julai 11.2022 ukumbi wa mikutano wa Halmashauri)

 Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO DC

Ushauri umetolewa kuundwa kwa sheria ndogo za Halmashauri kwa ajili ya kutekeleza agizo la serikali la kuwataka wazazi kuchangia chakula mashuleni ili kuwabana Wazazi na Walezi wanaokaidi agizo hilo hali inayochangia utoro kwa wanafunzi na kusababisha ufaulu hafifu.

Ushauri huo umetolewa na wajumbe wa Kamati ya Lishe Wilaya wakati wa kikao cha Kamati hiyo cha kujadili taarifa za robo ya nne kwa kipindi cha Aprili-Juni 2022 pamoja na kupitia viashiria vya mkataba wa Lishe kwa kipindi cha Julai 2021-Juni 2022, kilichofanyika Julai 12.2022 karika ukumbi wa Halmashauri.

(Kaimu Afisa Mipango (W). Ndugu Paulo Sangiwa (mwenye miwani) akifuatiwa na Afisa Elimu Maalum Mwalimu Peter Japhet na Kaimu Mkuu wa Idara ya 

Kilimo Ndugu Stephen Majumba)

Akichangia taarifa ya hali ya utoaji chakula shule za Msingi na Sekondari iliyowasilishwa na Mwalimu Peter Japhet kwa niaba ya Wakuu wa Idara za Elimu Msingi na Sekondari,  Afisa Habari Mawasiliano na Uhusiani Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Bwana Cosmas Njingo alisema ipo haja ya Idara hizo mbili kuona namna ya kuweka mkakati wa kutunga sharia ndogo kwa ajili ya kuwabana Wazazi na Walezi wanao kaidi agizo la Serikali la kuwataka kuchangia chakula ili kuwawezesha wanafunzi kupata chakula cha mchana mashuleni.

“Ushauri wangu kwa idara hizi mbili, zianzishe mchakato kupitia Ofisi ya Afisa Sheria wa Halmashauriwa kuandaa rasimu ya Sheria ndogo za kuwabana Wazazi na Walezi wanaokaidi kwa makusudi agizo halali la Serikali linalowataka wazazi wote kuchangia vyakula mashuleni kwa ajili ya watoto wetu”.

(Mratibu wa Lishe (W) Bi. Loveness Achimpota na Afisa Lishe wa Mradi wa Lishe Endelevu unaotekelezwa na Taasisi ya CEMDO Ndugu. John Kiussa)

Msemaji huyo kutoka Kitengo cha Mawasiiano Serikali cha Halmashauri, akaongeza kuwa kuwepo kwa sheria hiyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa migogoro ambayo inajitokeza hivi sasa kati ya Watendaji wa Kata, Walimu Wakuu pamoja na Wakuu wa Shule na Wazazi kutokana na kukosa nguvu za kisheria katika kuwachukulia hatua Walenzi na Wazazi ambao wamekuwa kikwazo kuhusu utekelezaji wa kuchangia chakula mashuleni.

“Ndugu wajumbe migogoro mingi imeibuka baina ya Wazazi na Watendaji wa Kata, Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu, kutokana na baadhi yao kukaidi kwa makusudi kuwachangia vyakula watoto wao, sasa kimsingi Watumishi hawa wanapata shida sana kutekeleza swala hili, maana hakuna sheria ya kuwalinda Watendaji na walimu, lakini pia hakuna sheria inayowapa meno kuchukua hatua kali dhidi ya Wazazi wanao kaidi amaelekezo ya Serikali”. Alieleza Bwana Njingo.

(wajumbe wa Kamati ya Lishe Wilaya, katika kikao cha Kamati Julai 11.2022 ukumbi wa mikutano wa Halmashauri)

Naye Mwakilishi wa Umoja wa Madhehebu ya Kikristo Tanzania (CCT), Peter Kihiyo alisema upo ulazima wa mchakato huo wa utayarushaji wa sheria ndogo kuhusu maswala ya lishe mashuleni na kwamba ufanyike haraka ili kunusuru hali ya ufaulu kwa wanfunzi.

“Mwenyekiti nakubaliana kabisa na mjumbe aliyetoa ushauri huu, ni muhimu utaratibu wa kuandaa Rasimu ya Sheria hii ukamilike haraka ili ipitishwe kwenye vikao vyote muhimu vya kisheria na ianze kutumika mara moja. Hii itasaidia kunusuru hali ya utoro mashuleni kwa wanafunzi kukosa chakula cha mchana”, alisisitiza.

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Lishe katika robo ya Nne ya kipindi cha Aprili-Juni 2022 Afisa Lishe Wilaya ya Gairo Bi. Loveness Achimpota alisema kuwa Lishe na Utapiamlo ni maswala mtambuka katika jamii na husababisha matatizo mengi.

(Mratibu wa Lishe (W) Bi. Loveness Achimpota) aliyesimama akiwasilisha mada, waliokaa kutoka kushoto ni Kaimu Katibu wa Mikutano Ndugu Abuu Liwangila na Afisa Habari Ndugu Cosmas Njingo)

“Lishe ina athari kubwa kwa makundi maalum kama watoto wa chni ya umri wa miaka mitano, wajawazito na akina mama wanaio nyonyesha. Hivyo ni wajibu wakila mjumbe kuhakikisha anawajibika kutoa elimu kuhusu maswala ya umuhimu wa Lishe kwa jamii ili kuepusha matatizo kama utapiamlo na vifo kwa watoto”, aliwasilisha Afisa huyo.

(Mratibu wa Lishe (W) Bi. Loveness Achimpota) aliyesimama akiwasilisha mada,

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa