• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KAYA 6271 ZA WALENGWA WA TASAF KUUNDA VIKUNDI 419 VYA KUWEKA AKIBA, KUWEKEZA WILAYANI GAIRO

Posted on: December 1st, 2021


Imeelezwa kuwa jumla ya kaya 6271 zinatarajiwa kushiriki kwenye uundaji wa vikundi vya kuweka akiba na kuwekeza kwa walengwa wa kaya zinazonufaika na mpango wa TASAF wa kusaidia kaya maskini Wilayani Gairo.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Bi Susan Nyanda amebainisha hayo kwenye hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo kwa timu ya wawezeshaji wa TASAF ngazi ya Halmashauri kuhusu utaratibu wa uundaji wa vikundi vya kuweka akiba na kuwekeza kwa walengwa wa Mpango, yaliyofanyika Disemba 1.2021 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

“Hapa Gairo tunzao kaya 6271 ambazo zimeingizwa kwenye utaratibu huu wa uundaji wa vikundi vya kuweka akiba na kuwekeza, lengo la Serikali ni kuhakikisha kaya zinajikwamua kiuchumi ili kujiongezea kipato”. Alisema Bi Nyanda.

Kaimu Mkurugenzi huyo akabainisha kuwa katika kipindi cha pili cha utekelezaji wa mpango huu mkazo umewekwa zaidi katika kuziwezesha kaya husika kufanya kazi ili kujiongezea kipato kupitia utekelezaji wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa Walengwa, pamoja na kuhamasisha  uwekaji wa akiba sambamba na kutekeleza shughuli za kukuza uchumi wa kaya hususani kwa kaya zenye uwezo wa kufanya kazi.

“Tunasisitiza kwamba ni wajibu kuhakikisha tunaweka mkazo mkubwa katika kuziwezesha kaya kufanya kazi, hasa zile kaya zenye uwezo wa kufanya kazi ilikujuiongezea kipatokupitia utekelezaji wa miradi inayotoa ajira za muda mfupi”, alisisitiza Bi Nyanda.

Bi. Nyanda akawaeleza washiriki wa mafunzo hayo kuwa katika kipindi kilichopita Kaya lengwa zilipewa elimu ya stadi za ujasiriamali na mbinu za uundaji vikundi endelevu vya kuweka akiba na kuwekeza, na kwamba zaidi ya Wanachama laki tatu wameunda vikundi vipatavyo 23, 6138 katika Halmashauri 78 Tanzania Bara na Visiwani.

“Kipindi kilichopita tulifanya uhamasishaji na utoaji wa eliku kwa jamii kuhusu uundaji wa vikundi vya kuweka akiba na kuwekeza, hapa Gairo kaya zilizohamasishwa zimeonyesha mwamko mkubwa na ari ya kuunda vikundi ili kutekeleza kwa vitendo elimu tuliyo itoa”, aligusia

Akaongeza kusema “Hapa kwetu Gairo tunatarajia kuunda vikundi vipatavyo 419 kutoka katika kaya 6271 ambapo kila kikundi kitakuwa na wanakikundi kati ya 10 na 15. Kupitia vikundi hivi kuna fursa za kukopa mikopo ya riba nafuu ambayo itasaidia kaya hizo kujikwamua kiuchumi kwa kuweka akiba na kuwekeza kwenye shughuli za uzalishaji mali”, Alibainisha Bi. Nyanda.

Mafunzo hayo ya siku tano yanaendeshwa na timu ya Wataalamu kutoka TASAF makao makuu yatafanywa kwa nadharia na vitendo ambapo Wawezeshaji ngazi ya Halmashauri watatakiwa kwenda kutoa elimu kwa jamii na kuhamasisha uundaji wa vikundi vya kuweka akiba katika vijiji vyao sambamaba na kushiriki katika shughuli za kukuza uchumi wa kaya.

Aidha wawzeshaji hao ngazi ya Halmashauri wametakiwa kukakikisha wanashirikiana na viongozi wa Wananchi ikiwepo Serikili za Halmashauri za vijiji, Wenyeviti wa vitongoji pamoja na Waheshimiwa Madiwani katika kata ambazo zoezi hili litatekelezwa.



Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa