• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MADIWANI WAONGEZE KASI YA USIMAMIZI WA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: June 3rd, 2024

Na, Cosmas Mathias Njingo. GAIRO 

Juni 3.2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Mhe. Rahel Nyangasi, amewaasa Wahe. Madiwani wa Halmashauri hiyo, kuongeza kasi ya usimamizi wa ukusanyaji wa mapato kwa kushirikiana na Maafisa Watendaji wa Kata, ili kufikia malengo ya ailimia 100 ifikapo Juni 30. 2024, kwa lengo la kuiwezwesha Halmashauri kupata mapato ya kutosha sambamba na kuhakikisha asilimia 10 zinarejeshwa kwa wakusanyaji wamapato kwa wakati.

Amesema hayo katika hotuba yake ya ufunguzi wa Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani wa kupokea na kujadili taarifa za Robo ya Tatu ya Januari- Machi 2023/024 uliofanyika Mei 24.2024 katika ukumbi mkubwa wa Mikutano wa Halmashauri.

“Malengo ambayo tumeyapanga wenyewe tukiyafanikisha inakuwa ni jambo jema sana, lakini pia tuwe tumefanikiwa kwa asilimia 100, ili tuingie mwaka mpya wa fedha 2024/2025 tukiwa na malengo mapya”. Alisema Mhe. Nyangasi

Hata hivyo Mhe.Nyangasi alisisitiza swala la kuwalipa kwa wakati Wakusanyaji wa mapato asilimia zao 10 ya kile wanachokikusanya linapaswa kutiliwa mkazo, kwani kwa kufanya hivyo kunatoa hamasa kwa wakusanya mapato kukusanya kwa bidi na uaminifu mkubwa, na kwamba utaratibu huo utaondoa wizi na njama za utoroshaji wa mazao kati yao na wafanyabiashara wanaosafirisha mazao.

“Kutokurejesha asilimia 10 kwa wakusanyaji ni Wizi, mtambue kuwa hela tunayoitumia kutekeleza shughuli mbalimbali za Halmshauri siyo yetu, ni fedha iliyopaswa kurudishwa kwa wakusanya ushuru. Hivyo tuhakikishe hili nalo tunalisimamia”. Alisisitiza.

Kwa upande mwingine Mhe. Mwenyekiti Amemshukuru Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuleta fedha nyingi za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo Wilayani Gairo, ambapo amewakumbusha Wahe. Madiwani hao kushiriki kwenye shughuli za maendeleo katika Kata zao, pamoja na kuhakikisha miradi yote ya maendeleo inatekelezwa kwa ubora unaotakiwa na ikamilike kwa Wakati.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa