• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MFUKO WA BIMA YA AFYA WAONGEZA HUDUMA ZA AFYA YA AKILI; WAZIRI UMMY

Posted on: October 11th, 2022

October 10th, 2022

Na WAF - DSM

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewataka Wataalamu wa afya kujadili uwezekano wa huduma za afya ya akili kuwa sehemu ya huduma zinazogharamiwa na mfumo wa taifa wa Bima ya afya ili kupunguzia mwananchi gharama za matibabu.

Waziri Ummy ameeleza hayo leo Oktoba 10, 2022 katika Kongamano la kwanza la kitaifa la afya ya akili lililofanyika katika kituo cha kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

“Suala jingine ambalo nataka kulijadili, ni kwanini Bima ya Afya isikubali kugharamia huduma za Saikolojia na huduma nyingine za Afya ya Akili zisiwepo kwenye Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya” amehoji Waziri Ummy Mwalimu.

Sambamba na hilo aliendelea kwa kuwataka Wataalamu katika Kongamano hilo kujadili namna bora ya kuboresha huduma na kutoa maoni ya nini kifanyike ili kukabiliana na changamoto za Afya ya Akili na kuboresha Huduma za Saikolojia na Afya ya akili ili kuwezesha wananchi kupata huduma bora.

Aidha, Waziri Ummy amesema bado kuna changamoto ya ajira kwa vijana na kuwataka wadau kushirikiana na Serikali kuanzisha vituo vya utengamao wa afya ili wananchi waweze kupata huduma za Saikolojia na Afya ya Akili karibu zaidi katika maeneo yao walipo.

Amesema, nchini Tanzania inakadiriwa kuwa na wagonjwa takriban milioni 7 wenye magonjwa mbalimbali ya akili na matumizi ya dawa za kulevya, huku akieleza kuwa, miongoni mwao zaidi ya watu milioni1.5 wanaishi na ugonjwa wa Sonona (Depression).

Nae, Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi amesema kufanyika kwa kongamano hili kutasaidia kupata michango tofauti kutoka kwa wadau muhimu wa afya ya akili juu ya fursa na changamoto zilizopo na kutoa mapendekezo ya kufikia suluhu ya utatuzi wa changamoto hizo.

Pamoja na hayo, Prof. Makubi amewashukuru na kuwapongeza timu yote ya maandalizi kwa kazi nzuri bila kusahau chama cha madaktari bingwa wa Afya ya Akili, Chama cha Wanasaikolojia na vyama vingine vya kitaaluma.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa