• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MKUTANO WA BARAZA LA KAWAIDA LA WAHE. MADIWANI KUPOKEA NA KUJADILI TAARIFA ZA ROBO YA PILI OKTOBA-DISEMBA 2023/2024

Posted on: February 9th, 2024

Na. COSMAS MATHIAS NJINGO, GAIRO

FEBRUARI 9.2024 

Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro, katika mwezi Januari 2024, ilipokea fedha kutoka Serikali Kuu jumla ya Shilingi Bilioni 1, 911, 450,910, kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo kwenye sekta za Elimu, Afya na Utawala; pamoja na kulipa malimbikizo ya Wastaafu.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bi. Sharifa Nabalang’anya, mbele ya Wahe. Madiwani; akimkaribisha Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Rahel Nyangasi, kufungua kikao cha Kawaida cha Baraza la Wahe. Madiwani; kilichoketi Februari 9.2024 kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

“Mhe. Mwenyekiti ninapenda kukijulisha kikao hiki cha Baraza la Wahemshimiwa Madiwani kuwa Halmashauri yeti imepokea Fedha kiasi cha Shilingi bilioni Moja nukta tisa moja, laki nne na hamsini elfu mia tisa na kumi kwa ajili ya matumizi ya miradi, malipo ya Wastaafu na malipo mengineyo”. Alisema Bi. Nabalang’anya.

Akitoa taarifa hiyo, Nabalang’anya alisema Shiling 1,256, 837,634 ni za mishahara ya Watumishi, wakati malimbikizo ya Wastaafu 4 ni Shilingi. 4,228,000 huku ruzuku ya matumizi ya kawaida ikiwa imetengewa Shilingi 72,086,000.

Mkurugenzi huyo wa Halmashauri alitaja zaidi matumizi mengine ya fedha hizo; kuwa ni pamoja na Shilingi 84, 219, 358 za Elimu bila ada kwa shule za Msingi na Sekondari, miradi ya ujenzi wa miundombinu shule za Sekondari kwa mwaka 2024 shilingi 319,086,000, Mfuko wa pamoja wa Afya (HSBF-CHMT) shilingi 113,615,750 na shilingi 61,464,168 kwa ajili ya Chanjo za kawaida, GAVI na Kovidi 19 ngazi za chini.

“Mhe. Mwenyekiti ninaomba kutumia nafasi hii kwa moyo wa dhati kumshukuru sana Mama yetu; Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwekeza mapenzi makubwa kwa Wananchi wa Gairo, hasa kutenga fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo”. Alishukuru Bi. Sharifa.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Nyangasi akifungua mkutano huo alisema, Wajumbe wa Baraza hilo la Wahe. Madiwani wamepokea kwa shukrani nyingi salam za upendo kutoka kwa Mhe. Rais Dkt Samia kupitia mgawo wa fedha hizo ambazo alibainisha zinaenda kuleta mbadiliko kwa Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo na kuchochea maendeleo.

Sambamba na shukrani hizo Mhe. Nyangasi aliwaasa Wakuu wa Divisheni na Vitengo na Watumishi wote, kufanya kazi kwa weledi, uadilifu, umakini na uaminifu wa hali ya juu, katika kusimamia utekelezaji wa shughuli za maendeleo ili kuleta matokeo chanya ya matumizi ya fedha hizo zilizotolewa na Serikali.

Baraza hilo mbali na mambo mengine, limepokea na kupitisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa kipindi cha Robo ya Pili cha Oktoba-Disemba 203/2024 huku likimsisitiza Mkurugrnzi wa Halmashauri na Timu yake ya Wataalam kuhakikisha maagizo yote yaliyotolewa yakatekelezwe kikamilifu.



Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa