• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

SERIKALI YAOMBWA KUISAIDIA HALMASHAURI KUFANYA TAFITI, UJENZI WA MABWAWA ILI KUTEKELEZA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

Posted on: October 30th, 2022

Na. Cosmas Mathias Njingo

GAIRO, Morogoro

Nov. 29.2022

 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Bi. Msifwaki Haule, ameiomba Serikali, kupitia Wizara ya Kilimo, kuisaidia Halmashauri hiyo kufanya tafiti na upembuzi yakinifu juu ya uchimbaji wa mabawa ili kuwezesha kilimo cha umwagiliaji ikiwa ni mkakati wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia Nchi.

Bi.Haule ametoa ombi hilo mbele ya Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Anthony Peter Mavunde (MB), wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki la Kilimo Gairo, lililohitimishwa kwenye kata ya Rubeho Oktoba 29.2022.

“Mhe. Naibu Waziri mabadiliko ya tabia Nchi yameleta athari kubwa kwa wakulima na kupunguza uzalishaji kutokana na ukame ambao umeikumba Wilaya yetu, kilimo chetu kinategemea mvua za msimu kwa kiasi kikubwa. Tunaiomba Wizara yako kusaidia katika kufanya utafiti wa uchimbaji wa mabwawa ili kuwezesha kilimo cha umwagiliaji”. Aliomba Kaimu Mkuirugenzi huyo.

Bi. Haule aliongeza kuwa kupitia tafiti hizo Halmashauri itabaini njia mbadala za kuendeleza kilimo kwa njia ya umwagiliaji, hali ambayo alieleza kuwa itaongeza uzalishaji wa mazao yenye tija, sambamba kuinua pato la wakulima na wafugaji.

“Kwa kufanya hivyo Mhe. Naibu Waziri, tafiti zitatuonyesha ni namna gani tunaweza tukatumia mabwawa hayo kuwekeza zaidi kwenye kilimo cha Umwagiliaji ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao na kusaidia kuinua pato la mkulima badala ya kuendelea kutegemea mvua za asili ambazo hazina uhakika sana, kutokana na mabadiliko ya tabia Nchi ambayo yameleta athari kubwa katika sekta ya kilimo”. Alifafanua Kaimu Mkurugenzi Bi. Haule.

Akihutubia mamia ya wakati wa Kata ya Rubeho walioshiriki kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki la Kilimo, Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe. Mavunde alisema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan imetenga kiasi cha shilingi Bil 400 kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji ambazo zimeelekezwa kwenye uchimbaji wa mabwawa na ujenzi maiundombinu muhimu katika mabwawa hayo.

“Bajeti ya Wizara ya kilimo imeongezeka kutoka Shilingi Bil.294 mwaka 2021/2022 na kufikia kiasi cha shilingi Bil.954 kwa mwaka wa fedha 2022/2023. Ambapo kati ya fedha hizo, kiasi cha shilingi nilioni mia nne zimelekezwa katika uchimbaji wa mabwawa na ujenzi wa miundombinu yote muhimu katika mabwawa hayo”. Asliesma Mhe. Mavunde.

Akaongeza kuwa dhamira ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha uzalishaji unaongezeka na kuwa wenye tija pamoja na kuwawezesha wakulima kuzalisha mara mbili kwa mwaka badala ya kuendelea kuzalisha mazao hafifu kwa kutegemea msimu wa mvua ambao ni mara mojwa kwa mwaka.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame akimkaribisha Mhe. Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde alisema, Wilaya ya Gairo imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha inatatua kero zinazowakabili wakulima na wafugaji ili dhamiria ya Mhe. Rais Samia ya kuleta mageuzi kwenye Sekta ya Kilimo ifikiwa.

Maadhimisho ya Wiki la Mkulima Wilaya ya Gairo, yalizindiliwa rasmi Oktoba 27.2022, na Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Jabiri Omari Makame, katika kata ya Ukwamani na kuhitimishwa Oktoba 29, 2022, ambapo Shughuli za maonesho ya bidhaa mbalimbali na teeknolojia za kilimo ziliendelea kufanyika na kuwapa fursa Wakulima kutembelea kwenye mabanda ya wadau wakilimo kujifunza ma kujionea shughuli zinazotekelezwa na Wadau hao.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa