• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

TANI 148,000 KUUZWA NJE YA NCHI: WAZIRI MCHENGERWA

Posted on: August 6th, 2023

Na. Cosmas Mathias Njingo, MOROGORO.

Agosti 6.2023

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb) amesema mwaka huu Serikali imepanga kuuza nje ya nchi tani 148,000 za asali hivyo amewataka wafugaji wa nyuki kuzalisha asali hiyo wa wingi ili kutimiza lengo hilo.

Waziri Mchengerwa ameyasema hayo Agosti 4 mwaka huu alipotembelea banda la Mtandao wa Vikundi vya Wakulima wadogo Tanzania (MVIWATA) katika viwanja vya Mwl. Julius Kambarage Nyerere vilivyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ikiwa ni siku ya nne tangu kufunguliwa kwa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki.

Waziri huyo amesema kwa sasa asali inayouzwa ni 5% tu hivyo Serikali kupitia Wizara hiyo imepanga kuongeza uzalishaji kwa kutoa elimu kwa wafugaji wa nyuki ili waweze kuongeza kiwango cha uzalishaji na kufikia zaidi ya asilimia 50% ya asali inayouzwa nje ya nchi.

“Tunauza asali nje ya nchi 5% mpango wetu wa Wizara ni kuuza tani 148,000 kwa mwaka huu, maana yake ni kwamba tuzalishe tani 148,000 tuongeze uzalishaji kutoka 5% ikibidi tufike hadi 50%” alsema Waziri Mchengerwa.

Aidha, Mchengerwa ameitaka benki ya Azania ambayo inatoa mikopo yenye riba nafuu ya 1% kwa Wanawake kutanua wigo wa utoaji wa huduma katika maeneo ambayo hayana matawi ya benki hiyo ili kila Mwanamke apate fursa ya kunufaika na huduma za mikopo hiyo.

Akitoa shukrani kwa Waziri huyo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ameahidi kuandaa mazingira mazuri ya kuhifadhia wanyama ambao wamekuwa sehem ya kivutio kikubwa cha maonesho hayo.

Sambamba na hilo, Mhe. Adam Malima amesema wataweka utaratibu ili maonesho hayo yasiishie kipindi cha Nanenane pekee utaratibu huo utawezesha maeneo hayo kuendelea kuwa kuvutio.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Saad Mtambule kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila amesema Kanda ya Mashariki inatafsiri kwa vitendo maelekezo na dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya uwekezaji katika sekta ya kilimo.

Kwa upande wake muwakilishi wa Meneja Benki ya Azania Mkoani Morogoro Bw. Josephat Mruma amesema benki hiyo kwa sasa inatoa mikopo ya 1% kwa wanawake ili waweze kujikita katika uzalishaji na kujikwamua kichumi.

Waziri Mchengerwa ametembelea mabanda mbalimbali yaliyopo katika viwanja hivyo na kujionea teknolojia mbalimbali ikiwa leo ni siku ya nne tangu kufunguliwa kwa maonesho hayo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa