• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAHE.MADIWANI WASHAURI HALMASHURI KURUDISHA ASILIMIA ZA WAKUSANYAJI MAPATO KWA WAKATI

Posted on: June 1st, 2024

Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO

Juni 1. 2024.

Baraza la Wahe. Madiwani wa Halmashuri ya Wilaya ya Gairo wameshaishauri Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kuweka utaratibu wa kuwapongeza wakusanya mapato na Kata zinazofanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato, hususani zilizovuka lengo la makusanyo ili kuongeza bidii ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri.

Wametoa ushauri huowakichangia taarahfa za mapato kwa kila Kata zilizowasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la kupokea na kujadili taarifa za maendelo ya kata kipindi cha Robo ya Tatu cha Januari Machi 2023/2024 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri mei 23.2024.


Diwani wa Kata ya Italagwe Mhe. Yosia akichangia hoja ya Mapato, ambapo amesisitiza kuwa ucheleweshaji kurudisha kwa asilimia za Vijiji na Kata ili kuwawezesha Halmashauri kupata Mapato mengi ya kutosha kutosha kuendeleza miradi mingine ya maendeleo inayoteklezwa kwa fedha za mapato ya Ndani.

Mhe Masatu Butindi Diwani wa Kata ya Kibedya, akichangia hoja hiyo, amepongeza Kata za Gairo na Rubeho kwa kuvuka lengo la makusanyo na kushauri kuwa kuwepo na utaratibu wa kutoa zawadi au kuziandikia barua Kata zilizofanya vizuri kwenye zoezi hilo la ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali.

Butindi ameikumbusha Halmashauri kuhakikisha fedha za madeni mbalimbali ikiwepo madeni ya Stahiki za Wahe. Madiwani, madeni ya Watumishi, Wazabuni na Watoa huduma mbalimbali wanalipwa kabla ya mfumo kufungwa ifikapo Juni.30.2023.


Kwa upande wake Mhe. Frank Mbaigwa Diwani Kata ya Ukwamani aliunga mkono hoja ya kuzipongeza kata zinazofanya vizuri katika zoezi la kukusanya mapato na kuongeza kuwa ni vyema pongezi hizo ziambatane fedha kidogo ilikuwatia moyo wakusanya mapato badala ya kuwaandikia barua peke yake za kuwapongezas

"Kata zinazofanya vizuri kwenye zoezi la ukusanyaji wa mapato zisiishie kuandikiwa barua za pongezi peke yake,barua hizo ziambatane na bahasha zenye chochote kitu ndani, hii itasaidia sana kuwatia moyo Watendaji wetu na kuongeza morali ya utekelezaji wa jukumu la kukusanya mapato. Na sisi Waheshimiwa Madiwani tufanye kama ilivyofanyika kwenye wiki la Elimu, Walimu waliofaulisha vizuri masomo yao walipongezwa kwa bahasha". Mhe. Frank Mbaigwa Diwani Kata ya Ukwamani.

Mhe. Mbaigwa alitoa ushauri huo kufuatia taarifa za Kata za Gairo na Rubeho kuvuka lengo la makusanyo kwa kipindi cha robo ya tatu zaidi ya 100% huku utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa Fedha 2023/2024 ukielekea ukingoni, ambapo kuanzia Julai Mosi 2024 Halmashauri itaanza kutekeleza bajeti ya mwaka mpya wafedha 2024/2025.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa